Tottenham wamekataa ofa ya mkopo wa pauni milioni 1.5 kutoka Paris St-Germain kwa ajili ya mlinda mlango Dele Alli na mchezaji huyo, 24, anajiandaa kuendelea kusalia kwenye klabu hiyo ya London. (Guardian)
Lakini klabu ya Ligue 1 watakuwa wanaandaa ofa ya mwisho ya mkopo kwa ajili ya Alli. (Telegraph)
Spurs pia imeweka ofa ya mkopo kwa ajili ya mlinzi Antonio Rudiger, 27, anayekipiga Chelsea, wakati mazungumzo yakiendelea kati ya mahasimu hao wa London. (Nicolo Schira via Express)
Arsenal wamekubali dili la mkopo kwa ajili ya mlinzi wa Uruguay Lucas Torreira, 24, kwenda Atletico Madrid, na hatua hiyo itawaruhusu kumsajili kiungo wa kati Hossem Aouar, 22, kutoka Lyon. (AS,via Mirror)
Paris Saint-Germain wanaweza kudhoofisha mpango wa washika bunduki kumshawishi Aouar baada ya pia kuingia kwenye mazungumzo ya kumnasa Mfaransa huyo. (L’Equipe,via Metro)
The post USAJILI: Wanaotikisa tetesi za usajili Ulaya appeared first on Bongo5.com.