Raia mmoja wa Italia, amekamatwa nchini Ufaransa, baada ya waranti ya kukamatwa kwake iliyotolewa na Ujerumani, ambako alikuwa akitafutwa kwa mashtaka 160 ya ubakaji au unyanyasaji wa kingono kwa watoto wadogo wa wenzi wake.


France arrests Italian over 160 child rapes, assaults | Daily Sabah


Mtuhumwa huyo wa umri wa miaka 52, alitiwa mbaroni Ijumaa iliyopita kusini mwa Strasbourg, eneo la karibu na mpaka wa Ujerumani.


Anahusishwa na uhalifu ambao inadaiwa aliufanya katika kipindi cha miaka 14 iliyopita kuanzia mwaka 2000.