Mchambuzi wa soka Abbas Pira amekimwagia sifa kikosi cha Mabingwa wa Nchi, Vijana wa Kariakoo Simba SC na kusema kuwa kikosi chao kipo vizuri mno huku akitumia maneno ya kiufundi zaidi katika kukisimulia. Abbas anaamini Mabingwa hao wa nchi bado wanayo nafasi ya kutetea ubingwa wao msimu huu wa 2020/21 kutokana na Ubora pamoja na Uimara wa kikosi hiko huku akiwatabiria kupata ushindani mkali kutoka kwa mtani wake wa Jadi Mabingwa wa Kihistoria Yanga kutokana na kufanya vizuri katika usajili wao pia. ”Simba imefanya usajili mzuri sana, hata Yanga pia msimu wacha tusubiri tuone naamini tutaona soka zuri sana kutoka kwao.”- Abbas Pira

IMEANDIKWA NA HAMZA FUMO, INSTAGRAM @fumo255

The post UCHAMBUZI: Simba kiufundi wapo vizuri, skills za Morrison na usajili (+Video) appeared first on Bongo5.com.