Mshambuliaji wa Aston Villa Mbwana Samatta rasmi amejiunga na klabu ya Fenerbahce ya nchini Uturuki.

Nyota huyo raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 27  alijiunga na Villans akitokea Genk mwezi Januari na kufunga jumla ya magoli mawili pekee kwenye michezo 16 aliyocheza chini kocha Dean Smith.

Kupitia kurasa za Aston Villa pamoja na zile za Fenerbahce zimethibitisha kujiunga kwa mshambuliaji huyo wa Tanzania.

”Ally Samatta amejiunga na klabu ya Fenerbahce ya Uturuki, bahati njema,” Ujumbe wa Aston Villa kwa Mbwana Samatta.

The post RASMI: Samatta atua Fenerbahce appeared first on Bongo5.com.