Na Samirah Yusuph, Simiyu.
Wajasiriamali wadogo wameshauriwa kutumia cliniki za kibiashara ili waweze kukabiliana na changamoto zinazopelekea kukwama na kuangusha biashara zao.

 Ushauri huo umetolewa na mratibu wa Cliniki hiyo Gilbert Waigama, amesema lengo la vituo hivyo ni kutibu matatizo ya biashara yanayozikabiri biashara zao.

Alisema licha ya kutatua kero mbalimbali zilizopo, pia wanajenga biashara kwa kuwapa wakulima elimu sitahiki ambayo itawaongezea uwezo na umahili katika kuendesha biashara.

"Tatizo kubwa ambalo wafanyabiashara katika Kanda nyingi ni namna ya kurasimisha wa biashara, hivyo mteja akifika hapa changamoto hizo zinapata ufumbuzi," alisema.

Cliniki ya biashara inaundwa na taasisi mabali mbali za kifedha, (za kiserikali na sekta binafsi) Kama SIDO, TANTRADE, TBS, na nyingine ambazo zinatoa huduma hizo.

Ambapo tangu wameanza kuhudumia wafanyabiashara 2018 Hadi 2020 wamewafikia wafanyabiashara 1200 kote nchini.