Rais wa Chama cha Wanamuziki wa Injili Tanzania, Dkt. Donald Kisanga amefariki dunia kwa ajali ya gari Jijini Dodoma alipokuwa akienda kugombea ubunge kupitia Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM).

Taarifa

Tanzania Music Foundation inasikitika kutangaza kifo cha Dkt. Donald Kisanga, Rais wa Tanzania Music Foundation kilichotokea leo kwa ajali ya gari alilokua akiendesha Jijini Dodoma.

Mwili wake umehifadhiwa HospitalI Dodoma.

Endelea kufuatilia taarifa za msiba huo zitakuwa zinatolewa mara kwa mara Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina la Bwana libarikiwe imetolewa na Stella Joel, Katibu Mkuu wa Tanzania Music Foundation.