“Kwa nini tulipe pesa kwa kutengeneza kitu kifupi kama hicho, sisi ni mashabiki wako ambao tunakufanya ujulikane kwani huwezi kufanya kwa upendo…’’
Aliandika shabiki mmoja. Kufuatia hali hiyo, Tanasha aliwajia juu na kuwaambia hakuna kitu cha bure hivyo wasimfikirie vibaya kwani kufanya vile ni kama kulipia kumuona msanii au kununua bidhaa.
“Mashabiki wasinifikirie vibaya, kulipia video ni kama vile unavyokwenda kununua bidhaa sokoni au kutoa pesa kwa ajili ya kuingia kwenye shoo ya kumuangalia msanii unayempenda,’’ alijibu Tanasha kwenye Insta Stori kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Stori: Happyness Masunga. Ijumaa