BAADHI ya Wakurugenzi wa Idara mbalimbali katika Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, wakifuatilia Kikao cha kuwasilisha ripoti ya Utekelezaji Mpango Kazi, kilichofanyika katika ukumbi wa IKulu Jijini Zanzibar, wakati ikiwasilishwa, kikao hicho kimeongozwa na Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein.
MSHAURI wa Rais Masuala ya Historian a Mambo ya Kale Mhe.Ali Mzee Ali, akichangia wakati wa Kikao cha Utekelezai Mpango Kazi kwa mwaka wa fedha 2020/2021, kilichofanyika Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)