Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amemtembelea Mjane wa Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Butiama mkoa wa Mara.

Dkt Mabula alikuwa katika ziara ya siku moja wilayani Butiama kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi sambamba na kugawa hati za ardhi kwa wananchi wa Butiama mkoani Mara waliopimiwa na kumilikishwa maeneo yao.

Naibu Waziri mbali na kutembelea wilaya ya Butiama pia alitembelea wilaya za Musoma, Rorya na Tarime ambako alizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi, alikagua mfumo wa ukusanyaji kodi ya pango la ardhi na kufuatilia maelekezo aliyoyatoa kuhusiana na masuala ya ardhi.