Mhudumu kutoka hospital ocean road akimhudumia mteja katika maonyesho ya nane nane Nyakabindi mkoani Simiyu.
 ***
Na Samirah Yusuph, Simiyu.
Taasisi ya saratani ya ocean road, imejikita katika kutoa elimu kwa wananchi dhidi ya mtindo Bora wa maisha ambao utawakinga dhidi ya saratani.

Mfumo wa maisha umetajwa kuwa ni sababu kubwa ya watu wengi kuungua sarati, kwa sababu ya kutokufuata misingi ya lishe bora Hali inayopelekea uzito uliopitiliza.

Akihimiza wananchi kufanya mazoezi pamoja na kutoa elimu juu ya saratani Dr. Maguha Stephano, alisema kuwa kufanya mazoezi pamoja na lishe bora ni moja ya Kinga ambayo inasaidia kulinda mwili.

"Inabidi wanachi waelewe namna ya kuweza kukabiliana na saratani lakini vilevile waweze kuelewa namna ya kuishi na saratani," alisema

Alisema kuwa kufika kwao Kwenye maonyesho ya nane nane ni pamoja na kuona wagonjwa wa kanda ya ziwa Ili waweze kuwahudumia, pamoja na kutoe elimu kuhusu saratani.

"Tunahimiza wananchi ili wapime Mara kwa Mara waweze elewe hatua za saratani na pia tunatoa chanjo za homa ya ini pamoja na saratani ya homa ya ini," aliongeza.

Hali ya maambuki ugonjwa wa saratani
Kwa takwimu za mwaka 2019 taasisi ya saratani ya ocean imebainisha kuwa Kati ya wagonjwa wote wanawake wa saratani ni 47%, saratani ya matiti 16% ,saratani ya utumbo mkubwa na mdogo ni 5.8%, saratani ya Koo 5.3% na saratani ya kichwa na shingo ni 4.2%.

Kwa upande wa wanamme saratani ya tezi dume ni 23%, saratani ya Koo 16%, saratani ya kichwa 12%, saratani ya utumbo ni 11.4%, na saratani ya matezi 9%.