Kampuni ya mawasiliano inayoongoza kwa kutoa huduma za kidigitali nchini, Tigo Tanzania inawakaribisha wadau na wateja wake pamoja na wananchi wote kwa ujumla katika banda lao lililopo viwanja vya maonesho ya biashara Sabasaba jijini Dar es Salaam ufurahie huduma mbali mbali na ofa kibao. Banda la Tigo lipo mkabala na banda la Wizara ya Viwanda na Biashara.