Rais Magufuli amemteua Gabriel Malata kuwa Wakili Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Julius Mashamba.


Kabla ya uteuzi Malata alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.

Aidha, Rais Magufuli amemteua  Boniface Luhende kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Malata.