Mbunge wa Iringa Mjini aliyemaliza muda wake kupitia CHADEMA Mchungaji Peter Msigwa, amesema kuwa aliamua kuwasikiliza wazee wa Mkoa huo, hii ni baada ya wao kumfuata na kumuomba aachane na nia yake ya kugombea Urais abaki kutumikia jimbo hilo.
"Nililazimika kutoendelea na mchakato wa Urais sababu Wazee na watu wa Iringa waliniomba sana na kunisihi bado niendelee kukaa kwenye jimbo , kwahiyo niliona nisikilize wazee na usia wao, nikaona niwapishe hawa wengine waendelee Mungu akiruhusu wakati mwingine nitarudi" amesema Msigwa.