Kundi la Waandamanaji limeangusha sanamu ya Christopher Columbus na kuitupa kwenye maji katika bandari mjini Baltimore hapo jana usiku
Waandamanaji wamekuwa wakitaka kuondolewa kwa masanamu mengi ya kihistoria yenye utata, ya watu wanaoelezwa kuhusika na ukandamizaji kwa karne kadhaa
Columbus anayesifiwa kwa kuligundua bara la Amerika, hivi karibuni wanahistoria na wanaharakati wamesema alihusika pia katika utumwa, unyonyaji na ukandamizaji pamoja na umwagaji damu wa watu