Rais Magufuli amemteua Kamanda wa Kikosi cha Polisi TAZARA, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advera John Bulimba kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nzega akichukua nafasi ya Godfrey William Ngupula
Aidha, Waziri wa Utumishi, Kept (Mst) George Mkuchika kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais Magufuli amemteua Omary Mwanga kuwa Katibu Tawala Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Husna Juma Sekiboko
Pia, Waziri Mkuchika amemteua aliyekuwa Afisa Tarafa Wilayani Mbulu, Saitoti Zelothe Stephen kuwa Katibu Tawala Wilaya ya Mbeya akichukua nafasi ya Hassan M. Mkwawa