Aliyewahi kuwa waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, leo Julai 19, 2020 amerejesha fomu za kuomba kuteuliwa kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya ACT Wazalendo.

Makabidhiano hayo yamefanyika Ofisi ya ACT Wazalendo Magomeni, jijini Dar es salaam ambapo amekabidhi fomu hizo kwa Naibu Katibu Mkuu Bara wa ACT Wazalendo Ndugu Joran Bashange.

Membe ambaye kauli mbiu yake alitaja kuwa ni Kazi na Bata, alikubali kuwania nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo, kwa kile alichodai kwamba huo ni wakati muafaka kwake wa kushiriki mazungumzo na vyama vingine ili waweze kusimamisha mgombea mmoja.