Aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, amekubali kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania kupitia ACT Wazalendo na kwamba huo ni wakati muafaka kwake wa kushiriki mazungumzo na Vyama vingine ili waweze kusimamisha mgombea mmoja.
Jana wakati akizungumza alisema haya “Mimi nimefukuzwa tena kwa aibu na kutukanwa na vijana ambao ningeweza kuwazaa, na sikutenda kosa lolote hata mbele ya Mungu, kosa nililofanya ni la kugombea Urais 2015, milango imefungwa na kufunguliwa na ACT na nikakaribishwa chumbani”.