Watu wanne wilayani Ukerewe, Mkoa wa Mwanza wamefariki huku wengine 27 wakijeruhiwa baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria katika Ziwa Victoria kupigwa na radi.
 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza ACP. Muliro Jumanne amesema, tukio hilo limetokea Juni 23 mwaka huu saa 2 na dakika 45 asubuhi katika Kitongoji cha Busele, Kata ya Bubiko, wilayani Ukerewe mkoani Mwanza.

Muliro amesema, mtumbwi huo wa abiri unaojulikana kama One Ten wenye namba za usajili 00238 unaofanya safari za Kome na Bugaza ulipigwa radi na kusababisha vifo vya watu wanne pamoja na majeruhi 27 ambapo kati yao ni wanawake 12 na wanaumme 15.

Alitaja majina ya waliofariki kuwa ni ;

1. Deogratus mulungu, miaka 50, mkara.
2. Kumunya andrea, miaka 36, mkerewe, mkristo,
Ambaye alikuwa ni nahodha wa mtumbwi.
3. Simon cherles, miaka 36, msukuma, mkristo,
Aliyekuwa nahodha msaidizi.
4. Ndege abdu, miaka 25, mjita, kibara.


Pia amesema, majeruhi wamefikishwa katika Zahanati ya Kijiji cha Bukiko na wengine Kituo cha Afya cha Bwisya kwa ajili ya matibabu, huku baadhi wametibiwa na kuruhusiwa. 


Amesema Miili ya marehemu wote imefanyiwa uchunguzi na daktari na kukabidhiwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.