Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mlipuko wa #CoronaVirus unaweza kusababisha vifo kwa Waafrika wapatao 190,000 ndani ya mwaka mmoja tangu uanze, kama ukishindwa kudhibitiwa.

World Health Organization Director-General Tedros Adhanom Ghebreyesus looks on during a press conference following an emergency talks over the new SARS-like virus spreading in China and other nations in Geneva on January 22, 2020. – The coronavirus has sparked alarm because of its similarity to the outbreak of SARS (Severe Acute Respiratory Syndrome) that killed nearly 650 people across mainland China and Hong Kong in 2002-03. (Photo by PIERRE ALBOUY / AFP) (Photo by PIERRE ALBOUY/AFP via Getty Images)

Mkurugenzi wa WHO-Afrika, Dkt. Matshidiso Moeti amesema kuna uwezekano kuwa #COVID19 haitosambaa kwa kasi barani humo kama ilivyokuwa kwa mataifa mengine duniani.

Hata hivyo, amezitaka Serikali kuweka mikakati ya kupima #Corona, kuwatibia wagonjwa, kuweka wenye maambukizi karantini na vilevile kutafuta wale waliokuwa karibu na wagonjwa wa Virusi hivyo.

Awali, WHO ilitabiri Waafrika Milioni 29 hadi 44 wanaweza kupata #COVID19 kwa mwaka mmoja na Milioni 5.5 wanaweza kuhitaji tiba Hospitali, idadi ambayo ni kubwa kuliko uwezo wa sekta za afya katika nchi nyingi.

The post WHO: Waafrika 190,000 wanaweza kufa kwa mwaka kutokana na Corona appeared first on Bongo5.com.