Mchungaji kiongozi wa Kanisa la Warehouse Christian Center(WHC), Dkt. Peter Mitimingi amefafiki usiku wa kuamkia leo. Mchungaji Msaidizi wa kanisa hilo Samwel, amethibitisha. 

Mpaka anafariki alikuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Huduma ya the Voice of Hope Ministry, Mshauri wa Saikolojia wa BLCCC.

Alifahamika zaidi kwa mahubiri na mafundisho yake kuhusu mahusiano na maisha ya ndoa yaliyoenea zaidi kupitia Mitandao ya Kijamii.