Marekani imeendelea kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya vifo vinavyotokana na corona Duniani ambapo hadi mchana huu idadi ya waliofariki  imefika 45,343.

Marekani pia inaongoza kwa visa, vimefikia 819,175  na wamepona 82,973

Jana Jumanne Marekani ilirekodi vifo 2,750 kwa siku licha ya takwimu mpya kuonesha maambukizi ya kila siku yanapungua nchini humo. 

Majimbo ya New Jersey, Pennsylvania na Michigan kila moja liliripoti vifo vya zaidi ya watu 800 kwa siku, huku jimbo la New York lililo kitovu cha mlipuko wa virusi vya corona nchini Marekani lilirekodi vifo vya watu 481.