Mbunge wa Jimbo la Sumve Wilayani Kwimba mkoani Mwanza, Richard Mganga Ndasa amefariki dunia mapema leo Mkoani Dodoma, Tanzania.
Ndassa ameanza kuwa Mbunge tangu mwaka 1995 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Spika Ndugai athibitisha kifo cha mbunge Richard Ndasa.
Mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndasa amefariki dunia jijini Dodoma usiku wa kuamkia leo.
Spika wa Bunge, Job Ndugai amethibitisha.
Shughuli za Bunge zimeahirishwa kwa siku ya leo kwa mujibu wa kanuni kwa maombolezo
The post TANZIA: Mbunge Ndassa afariki dunia Dodoma, Spika athibitisha appeared first on Bongo5.com.