Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob ametangaza kutogombea tena nafasi ya udiwani wa kata ya Ubungo katika uchaguzi ujao unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2020 nchini Tanzania.
 
Boniface Jacob ametangaza uamuzi huo kupitia mtandao wake wa Twitter 

 “Nimetangaza kung'atuka ktk udiwani kata ya Ubungo muda wa madiwani utakapo isha, sitogombea tena udiwani uchaguzi ujao..! Miaka 10 utumishi wangu ni kwa sababu Wana-Ubungo mlinikopesha imani. Tumekuwa wote wakati wa shida na raha, mabonde na milima.” Ameandika