Kutokana na kauli iliyotolewa na madaktari wawili wa kifaransa ambao ni Dk. Jean-Paul Mira pamoja na Camille Locht kusema kuwa bara la Afrika linafaa kwa vipimo vya corona hadi kupelkea wachezaji wakongwe Didier Drogba na Samuel Etoo kukemea vikali kauli hiyo.
Leo Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dr. Tedros ambae ni Raia wa Ethiopia, amekasirishwa na kauli hiyo ya kibaguzi iliyotolewa na Madaktari hao wa Ufaransa waliokuwa kwenye kipindi cha TV na kusema kuwa.
“Afrika haiwezi kuwa uwanja wa majaribio ya chanjo ya corona, tutafuata taratibu zote kufanya majaribio ya chanjo Duniani kote iwe ni Ulaya au Afrika kwa usawa, hizi fikra za kikoloni zikome, wote ni Binadamu ”
By Ally Juma.
The post Kauli za madaktari wa Kifaransa zafika WHO na kutoa kauli ” Fikra za kikoloni zikome, Afrika haiwezi kuwa uwanja wa majaribio ya chanjo ya Corona” – Video appeared first on Bongo5.com.