Wakati huo huo shirika la afya ulimwenguni WHO likionya dhidi ya “kuwapo kwa dhana ya uimara ya mwili” kwa wagonjwa wanaopona, kunakoonekana kuwa ni chombo cha mataifa kujitayarisha kufungua uchumi wao.
WHO inapinga, “hati” hizo kwasababu kupona kutokana na maambukizi ya virusi vya corona huenda kusimlinde mtu kutopata maambukizi tena.
“Kwa sasa hakuna ushahidi kwamba watu ambao wamepona kutokana na maambukizi ya COVID-19 na wana chembe cha kingamwili wana uwezo wa kulinda dhidi ya kupata maambukizi mengine,” shirika hilo la afya la umoja wa Mataifa limesema katika taarifa.
Wakati huo huo mamia ya mamilioni ya Waislamu duniani kote hawakuingia katika misikiti katika siku ya pili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuepuka kula pamoja kwa makundi katika familia wakati wa iftar kwasababu ya sera za kutokaa pamoja na kuweka umbali kati ya mtu na mtu.
The post Idadi ya vifo vya COVID – 19 yafikia 200, 000 Duniani, WHO yaonya juu ya dhana hii appeared first on Bongo5.com.