Serikali imeiagiza Tume ya Ushindani wa Kibiashara na Shirika la Ubora wa Viwango (TBS) kufanya msako na kuwachukulia hatua wafanyabiashara watakaobainika kuongeza bei kwa makusudi kwa lengo la kujipatia faida kubwa katika kipindi hiki kigumu cha mapambano dhidi ya virusi vya Corona.

Agizo hilo limetolewa leo Machi 21, 2020 na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa ambapo pia amewaonya wafanyabiashara walioficha bidhaa za vitakasa (sanitizers) na barakoa (mask) kuacha mara moja huku akiwatoa hofu Watanzania kuhusu upatikanaji wa bidhaa hizo na kuongeza kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha bidhaa zinapatikana kirahisi na kwa bei nafuu.

Chanzo Azamtv.

View this post on Instagram

WANAOONGEZA BEI ZA VIFAA KINGA DHIDI YA CORONA KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA: Serikali imeiagiza Tume ya Ushindani wa Kibiashara na Shirika la Ubora wa Viwango (TBS) kufanya msako na kuwachukulia hatua wafanyabiashara watakaobainika kuongeza bei kwa makusudi kwa lengo la kujipatia faida kubwa katika kipindi hiki kigumu cha mapambano dhidi ya virusi vya Corona. Agizo hilo limetolewa leo Machi 21, 2020 na Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa ambapo pia amewaonya wafanyabiashara walioficha bidhaa za vitakasa (sanitizers) na barakoa (mask) kuacha mara moja huku akiwatoa hofu Watanzania kuhusu upatikanaji wa bidhaa hizo na kuongeza kuwa Serikali inafanya kila linalowezekana kuhakikisha bidhaa zinapatikana kirahisi na kwa bei nafuu. #CORONA #CoronaTanzania #TahadhariCorona

A post shared by Azam TV (@azamtvtz) on

The post Wanaoongeza bei vifaa vya kujikinga na Corona kuchukuliwa hatua za kisheria appeared first on Bongo5.com.