Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ametembelea mnada wa mifugo wa Pugu na soko la samaki ferry jijini Dar es Salaam na kutoa agizo la serikali kwa wakurugenzi wote nchini kutofunga minada ya mifugo na samaki kwa sababu ya maambukizi ya virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa Covid – 19, badala yake amewataka kushirikiana na watalaamu wa afya ili kuhakikisha shughuli zinazofanywa katika minada hiyo zinafanywa kwa tahadhari ikiwemo ya watu kunawa mikono wakati wa kuingia na kutoka katika minada hiyo kwa kutumia maji tiririka yenye dawa.