Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amthibitisha Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) Brig. Jenerali John Mbungo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo baada ya kuokoa Shilingi Bilioni 8.8 za wakulima.

Rais Dkt. Maguguli Amechukua uamuzi huo baada ya kupokea ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) na ripoti ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mapema leo katika Ikulu ya Chamwino Jijini, Dodoma.