Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli  anakabidhiwa   Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2018/2019 inayowasilishwa na Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa Hesabu za Seriakali (CAG) Charles Kichere.

 Aidha Mhe. Rais atapokea Ripoti ya taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2018/2019 itakayowasilishwa na Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Taasisi hiyo Brigedia Jenerali John Mbungo . 

Hafla inayofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Ikulu Chamwino Jijini Dodoma Machi 26, 2020.