Burundi imedai watu wanaotumia mtandao wa internet kusema nchi hiyo haina vifaa vvya kugundua virusi vya corona kuwa ni waongo.

Kwenye taarifa iliyotolewa jana jioni, msemaji wa serikali ya Burundi Prosper Ntahorwamiye amesema nchi hiyo ina vifaa vya kutosha na vyenye ufanisi vya kugundua virusi vya corona. 

Ametolea mfano ushahidi kuwa mwalimu kutoka shule inayomilikiwa na Wafaransa aliyeshukiwa kuwa na virusi hivyo amepimwa, lakini matokeo yameonesha kuwa hana virusi.

Serikali ya Burundi imeonya dhidi ya vitendo vya kupotosha ukweli na kutafsiri vibaya maamuzi yaliyotolewa na serikali. 

Msemaji huyo amesema serikali ina madaraka ya kuchukua hatua mwafaka dhidi ya watu wanaotoa kauli zisizo za kweli.

Wakati huohuo, serikali ya Burundi imeshukuru China kwa kutoa vifaa vya kuisaidia kukabiliana na uwezekano wa mlipuko wa virusi vya Corona nchini humo.

Credit: CRI