Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa idadi ya wagonjwa wa Virusi vya Corona nchini imeongezeka na kufikia watatu, ambapo mmoja amepatikana Zanzibar ambaye ni raia wa Ujerumani na mwingine Jijini Dar es Salaam ambaye ni raia wa Marekani.

“Tuna ongezeko la wagonjwa wawili ambao wamethibitika kuwa na corona Tanzania, mmoja kutoka Zanzibar yeye ni Mjerumani ana miaka 24 na tayari yupo kwenye uangalizi, na hapa Dar tuna Mmarekani mwenye miaka 61 amebainika kuwa na corona pia” -Amesema Waziri Mkuu Majaliwa

Pia amesitisha masomo kwa vyuo vikuu na vya kati nchini kuanzia leo March 18, 2020 ili kukabiliana na Virusi vya Corona