Afrika Kusini imeanza kutekeleza leo amri ya watu kubakia majumbani mwao chini ya uangalizi wa jeshi, na kujiunga na nchi nyingine za Afrika zinazoweka hatua kali za watu kutotoka nje na kufunga shughuli nyingi katika jitihada za kusitisha kusambaa kwa virusi vya corona.

Watu milioni 60 nchini Afrika Kusini watalazimika kukaa nyumbani kwa siku 21.

Afrika Kusini ina visa 927 vya maambukizi ya virusi vinavyo sababisha ugonjwa hatari wa Covid-19 (Corona).

Hatua hizo zilitangazwa Jumatatu jioni na Rais Cyril Ramaphosa, ambaye alisema anataka kuzuia mlipuko wa janga la Covid-19 na kuepuka janga la kiafya.
 

"Kaeni nyumbani.... Baa, migahawa, maeneo ya starehe, mbuga, makanisa vimefungwa. Hakuna gari inyopaswa kutembea katika mitaa ya nchi hiyo.

"Maafisa pekee wanaofanya kazi katika sekta muhimu ndo ambao wanaruhusiwa kwenda kazini: hospitali, maduka ya dawa, maduka makubwa, maduka ya chakula. Watu wanaofanya kazi katika sekta za maji na umeme wanaweza pia kwenda kazi. Wafanya kazi katika sekta ya migodi ya makaa ya mawe, wataendelea kuripoti kazini.

"Ni marufuku mtu kutoka nje, barabarani, kwenda sehemu anakotaka," ameonya Waziri wa Polisi Mbeki Cele.