Muigizaji maarufu wa Tanzania Mwijaku aliongea kuhusu uhusiano wa Tanasha na msanii Diamond, si hayo alisema Diamond kumuoa mpenzi wake anahitaji miujiza.

Ni mahusiano ambayo mashabiki wanasema kuwa mapenzi yao yamenoga baada ya kutoa wimbo wao wa’gere’



Kulingana na mwijaku Diamond atamuacha Tanasha na kuenda katika mwanamke mwingine na mtindo huo kuendelea vivyo hivyo bila ya hata kujali.

“Diamond Kumuoa Tanasha ni miujiza itafanyika, hii ni kwa sababu mbili ambazo Diamond hajamaliza kufanya kwanza Diamond hajamaliza kuzunguka humu nje akiwachumbia wanawake

Ana karibu miaka mitano, Tanasha ataenda na mwanamke mwingine aje katika maisha ya Diamond na pia yeye atoke.” Alieleza Mwijaku.


Alimtetea Diamond na kusema,

” Hiyo si dhambi bado yupo na umri mdogo na amekubaliwa kufanya hivyo.” Alisema.

Wimbo ambao wameutoa juzi Tanasha anamwambia mpenziwe asijaribu kumuacha kwa sababu ya wanawake wengine na pia ana mwambia awaambie kuwa Diamond ni wake.

Aliangukia! Dhibitisho kuwa Zari kumuacha Diamond ulikuwa uamuzi bora

Kuna nyimbo kadhaa ambazo Diamond anadaiwa kuiba kutoka kwa wasanii wengine zikiwemo Kwangaru,Inama na Tetema.

Tanasha si mwanamke wa kwanza kuachwa na msanii Diamond kwa hivyo anapswa kuwa tayari kwa tukio lolote lile.

READ MORE: