Maendeleo ya Ujenzi wa Barabara za Juu katika Makutano ya Ubungo (Ubungo Interchange). Mradi huo wa Ujenzi katika Makutano ya Barabara za Mandela, Morogoro na Sam Nujoma (Ubungo Interchange) unaendelea kwa kasi kubwa na umefikia asilimia 65 kwa mradi mzima na sehemu ya gorofa ya pili ambayo itapitisha magari yanayotumia barabara ya Morogoro imefikia asilimia 75. Mradi huo unatarajiwa kuondoa adha ya msongamano mkubwa katika makutano ya barabara hizo pindi utakapokamilika. 
Ujenzi wa reli ya kisasa SGR
Upanuzi wa Barabara ya Morogoro kwa njia nane kuanzia Kimara –Kibaha unaendelea kwa kasi kubwa kama inavyoonekana pichani katika maeneo ya Kimara, Mbezi na Kibamba hivyo kuanza kupunguza msongamano mkubwa wa magari katika barabara hiyo ya Morogoro. 
Barabara ya Bagamoyo ambayo inaendelea kufanyiwa upanuzi
Barabara zilizoboreshwa kwenye makazi ya wakazi wa maeneo yasiyopimwa jijini Dar es Salaam. (PICHA NA IKULU).