Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt.Anna Mghwira akizawadiwa samaki aina ya Kambare na mwanakijiji wa Suwa Wilayani Handeni Mkoani Tanga. Dkt Mghwira yupo ziarani Handeni kujifunza na kujionea athari ya mafuriko ya mvua yaliyotokea hivi karibuni Mkoani Tanga. Bwawa la Suwa limeathirika kwa kiasi kikubwa sana ambalo ni chanzo cha maji Handeni vijijini.Picha na Jamal Zuberi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tanga (OMM-Tanga)