Rais John Magufuli amemuapisha Charles Kichere kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) akichukua nafasi ya Prof. Mussa Assad aliyemaliza muda wake leo Novemba 4, 2019. CAG Kichere alikuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Njombe na kabla ya hapo alikuwa Kamishna Mkuu wa TRA.