Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (katikati) akikata utepe kuashiria ufunguzi wa maonesho ya pili ya Sido Kitaifa 2019 yaliyofanyika Uwanja wa Bombadia Manispaaya Singida. Kutoka kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mussa Sima, Mke wa Waziri Mkuu Mary Majaliwa, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi Stellah Manyanya, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida, Alhaji Juma Killimbah, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara, Ludovick Nduhiye na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) Profesa Mhandisi Sylvester Mpanduji.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na viongozi wengine wakipiga makofi baada ya uzinduzi huo.
Raia wa Burundi walioshiriki maonesho hayo wakiwa wamekaa kwenye bidhaa zao wanazo zitengeneza.
Wajasiriamali wanaouza bidhaa za nguo na vitenge wakiwa katika banda lao.Kutoka kulia ni Anna Mtaturu kutoka Kiwauuku Textile and Garments Mkoa wa Singida, Rose Mapunda kutoka Goldenfay Asili Productd Textile and Garments, Mary Mayala kutoka Mary Garments na Mary Muhere kutoka Muhere Orginal Products (Textile and Garments)
Mjasiriamali Mary Muhere akiwa mbele ya bidhaa zake katika maonesho hayo.
Mjasiriamali Mary Muhere akiwa mbele ya bidhaa zake katika maonesho hayo.
Wafanyakazi kutoka Shirika la Sema mkoani Singida wakiwa mbele ya banda lao katika maonesho hayo. | . |
Wauzaji wa dawa za asili wakiwa kwenye banda lao.
Mwenyekiti wa Singida Sanaa Group, Ally Abushiri na Mjumbe wa kundi hilo, Chawala Philemon wakiwa wameshika picha waliyochora sura ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika maonesho hayo.
Wajasiriamali Matrida Lugeha (kushoto) na Catherine Nyasa kutoka Maty Fashion ( Textile) wakiwa mbele ya banda lao.
Mjasiriamali Aika Teri kutoka Nuya Fashions akiwa katika banda lake kwenye maonesho hayo.
Mjasiriamali Jesca Lema (kulia) anayetengeneza vishikio vya funguo akimuonesha Benard Ntiyakamo vishikio hivyo katika maonesho hayo. Kushoto ni Mjasiriamali Glory Lema.
Mjasiriamali Abbas Mwinyi kutoka Hiruma Gr oup la Urambo Singida akiwa mbele ya bidhaa zake pamoja na mtego wa kunasia watutu wa halibifu wa mimea michanga.
Wajasiriamali Frank na James Kimaro kutoka Kampuni ya Tesha Sofa Vunja bei ya mjini Singida wakiwa na bidhaa zao kwenye mao nesho hayo.
Wauza dawa za asili wakiwa katika banda lao.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA) wakiwa kwenye banda lao.
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ( TCRA) wakiwa kwenye banda lao.
Afisa Mawasiliano na Mahusiano ya Umma wa Tume ya Ushindani (FCC) Adefrida Ilomo akimuelekeza jambo mwananchi aliyetembelea banda la FCC.
Wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiwa kwenye banda lao katika maonesho hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Standard Radio FM ya Mjini Singida, James Daud (mwenye koti) akiwa na wafanyakazi wake katika banda lao kwenye maonesho hayo.
Afisa Masoko wa Benki ya Biashara Tanzania (NBC ) , Brigitha Benard (kulia) akimuhudumia Alfred Mauma baada ya kutembelea banda la benki hiyo kwenye maonesho hayo.
Wafanyakazi wa Benki ya NBC wakiwa kwenye banda lao kwenye maonesho hayo.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Luciana S.Hembe akiwa na wafanyakazi wa Taasisi hiyo Tawi la Singida katika uzinduzi wa maonesho hayo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Idara ya Tafiti Ushauri na Machapisho wa TIA, Gorah Abdallah, Afisa Masoko na Mahusiano ya Umma, Caroline Mulungu, Mhadhiri Msaidizi wa TIA, Eliaichi Kyara, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano kwa Umma TIA, Lillian Mpanju Rugaitika na Mdhibiti Ubora wa Elimu Tawi la TIA Singida, Daniel Mgonja.
Mjasiriamali Lucas Sagoda (kushoto) kutoka Dosin Products akizungumza na wanafunzi waliotembelea banda lake katika maonesho hayo.
Mawakala wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) wakiwa kwenye banda lao kwenye maonesho hayo.
Mfanyakazi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Liziki Salum (kushoto) akimpima shinikizo la damu Vivian Mlau baada ya kutembelea banda la NHIF ambapo zilikuwa zikitolewa huduma za kupima Kisukari, Urefu, Uzito na Presha.
Dkt.Filbert Shayo wa NHIF akizungumza na Ester Kiula baada ya kumpima kisukari.
Banda la NHIF lilivyokuwa likionekana kwenye maonesho hayo.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Efta Equipment Loans, Lazaro Stephen akizungumza na wananchi waliotembelea banda la kampuni hiyo yenye makao yake jijini Dodoma.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Efta Equipment Loans wakiwa ndani ya banda lao katika maoenesho
hayo.
Afisa Utawala wa Chuo Kikuu Huria (OUT) Yusuph Ngalemwa (kulia) akizungumza na wananchi waliotembelea banda la chuo hicho katika maonesho hayo. Wa pili kulia ni Mhadhiri wa chuo hicho, Bernard Komba.
Afisa Utawala wa Chuo Kikuu Huria (OUT) Yusuph Ngalemwa akizungumza na Mzee Zahoro Lyasuka aliyetembelea banda la chuo hicho katika maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (hayupo pichani) akisubiriwa kupokelewa kabla ya uzinduzi wa maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi mbalimbali baada ya kuwasili Uwanja wa Bombadia kufungua maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisaini katika kitabu cha wageni katika banda la Shirika la Viwango Tanzania (TBS)
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisalimiana na Muelimishaji Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Japhary Hamisi alipotembelea banda la Mamlaka hiyo katika maonesho hayo.
Kushoto ni Zakaria Gwagilo Afisa wa TRA Mkoa wa Singida.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wafanyakazi wa Standard Radio FM ya Mjini Singida baada ya kufungua maonesho hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade), Edwin Rutageruka (kulia) akimuelekeza jambo Waziri Mkuu alipotembelea banda la Benki ya Biashara ya NBC la Kliniki ua Biashara lililokuwepo kwenye maonesho hayo.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakiimalisha ulinzi wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akitembelea mabanda.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na Mwanasheria na Ofisa Mlinda Mlaji wa Tume ya Ushindani (FCC) Exavery Ngelezya (kushoto) alipotembelea banda la tume hiyo katika maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mbegu za alizeti alipotembelea banda la wazalishaji wadogo wa mafuta ya alizeti wa Mkoa wa Singida.
Mjasiriamali Pendo Chitinde kutoka Dodoma Mara Leather Products akimueleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusu bidhaa za ngozi zitazotengenezwa na kiwanda hicho.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia viatu vilivyotengenezwa na wajasiriamali waliopata mafunzo kutoka Chuo cha Veta.
|
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiangalia mashine zinazotengeneza bidhaa za ngozi.
Meneja Masoko wa Deve General Supplies Company, Gisela Denis (kushoto) akimueleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa changamoto ya soko la kuuza vifaa tiba vinavyotengenezwa na kampuni hiyo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisoma orodha ya vifaa tiba vinavyo tengenezwa na kampuni hiyo. Kulia ni mke wake Mary Majaliwa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza baada ya kuona vitanda vya wagonjwa na vya kujifungulia wajawazito vinavyotengenezwa na kampuni hiyo.
Wananchi wakisubiri kusikiliza hutuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya ufunguzi wa maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa meza kuu kabla ya kufungua maonesho hayo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi na kushoto ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Mhandisi Stellah Manyanya.
Ulinzi ukiimalishwa wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipokuwa akihutubia.
Wakina mama wakishangia wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akihutubia.
Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa maonesho hayo.
Kwaya ya AICT ya Singida Sabasaba ikitoa burudani wakati wa hafla ya uzinduzi wa maonesho hayo.
Sehemu ya umati wa watu waliokuwepo kwenye hafla hiyo.
Afisa Masoko wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Gladnes Kaseka (kulia) akimkabidhi mfuko wa kuwekea tairi la akiba Mkurugenzi Mtendaji wa Kisimbo and Sons Since 1985 Tanzania LTD. Wa pili kushoto ni Mkaguzi wa TBS, Domisiano Rutahala na Dereva wa TBS, Benjamin Mwingira.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB Mkoa wa Singida wakiwa kwenye banda lao kwenye maonesho hayo.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi cheti cha udhamini wa maonesho hayo Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kati, Nsolo Mlozi.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB wakionesha cheti cha udhamini wa maonesho hayo baada ya kukabidhiwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi cheti cha udhamini wa maonesho hayo, Afisa Masoko wa Kampuni ya Helvetas Tanzania, John Mabagalu.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Helvetas wakionesha cheti cha udhamini wa maonesho hayo. Wadau wa maendeleo 10 walitunukiwa vyeti hivyo vya udhamini.