Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu kazi , vijana na ajira, Anthony Mavunde(kushoto), akimkabidhi ruzuku ya komputa na vifaa vingine nya ofisini kwa Halima Haji Sasya, ambaye ni mmoja wa wanawake 256 ambao walipokeamafunzo ya uendeshaji na usimamizi wa biashara kupitia programu ya 2jiajiri.Wengine katika picha ni Mkurugenzi Mkuu wa KCB Foundation, Jane Mwangi(kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya KCB, Cosmas Kimario(wa pili kushito).

Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu kazi , vijana na ajira, Anthony Mavunde(kushoto), akimkabidhi ruzuku ya gari aina ya kirikuu kwa Janeth Kipangula,mfanya biashara wa vifaa vya ujenzi wakati wa ambaye ni mmoja wa wanawake 256 ambao walipokea mafunzo ya uendeshaji na usimamizi wa biashara kupitiaprogramu ya 2jiajiri. Wengine katika picha ni Mkurugenzi Mkuu wa KCBFoundation, Jane Mwangi (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya KCB,Cosmas Kimario(kulia).
 
Mwakilishi wa vijana wanaopokea mafunzo kutoka VETA na kudhaminiwa na Benkiya KCB, Nd. Baraka Konkara,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Programu yaKCB 2jiajiri Youth Scholarship kwa vijana inayoendeshwa na VETA nakudhaminiwa na Benki ya KCB katika hafla ya uzinduzi huo umefanyika jijini Dares Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Biashara ya KCB, Cosmas Kimario,
akizungumza wakati wa uzinduzi wa Programu ya KCB 2jiajiri Youth Scholarshipkwa vijana inayoendeshwa na VETA na kudhaminiwa na Benki ya KCB katika haflaya uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu kazi , vijana na ajira, Anthony Mavundeakizungumza wakati wa uzinduzi wa Programu ya KCB 2jiajiri Youth Scholarshipkwa wanafunzi wa Veta yaliyodhaminiwa na Benki ya Biashara ya KCB hafla yauzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam.

NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde amewataka vijana kuondokana na dhana ya kwamba ili waonekane wana ajira

lazima wafanye kazi ofisini badala yake amewaasa wajiajiri na kufanya biashara.

Mavunde amesema kuwa Serikali inatarajia ifikapo mwaka 2025, asilimia 40 ya nguvu kazi ya nchi ambayo ni vijana itakuwa imeajiriwa katika sekta ya viwanda.

Akizungumza jijini Dar es Salaam katika hafla iliyowakutanisha vijana zaidi ya 100 Waliochanguliwa kujiunga na programu ya Vijana 2jiajiri inayoratibiwa na Benki ya KCB,

Mavunde amesema Serikali inatengeneza mazingira wezeshi kwa vijana yatakayowasaidia Kuweza kujiajili na wengine kuajiliwa na kuongeza kuwa ukuaji wa viwanda nchini utafanikisha jambo hilo.

Amesema pamoja na serikali kutengeneza mazingira hayo vijana wanapaswa kuondokana na dhana ya kufikiria kwamba ili waonekane wana ajira ni lazima wafanye kazi maofisini badala yake amewataka wahakikishe wanajiajiri.

" Tatizo vijana wengi wanafikra mbaya ya kuajiriwa na wanawaza kuwa lazima wavae chati jeupe asubuhi suruali nyeusi na kwenda ofisini, mimi nawaomba wabadirike na waondokane na fikra hiyo kuanzia sasa, mnapaswa kujiajiri jamani kwa kufanya shughuli yeyote inayowaingizia kipato," amesema Mavunde.

"Tafiti za mwaka 2014 zinaonesha nchi inauwezo wa watu Milioni 24.3 wa kufanya kazi hivyo watu hawa kila mwaka wanaingia katika soko la ajira, kwahiyo wewe kijana ukikaa

nyumbani na kujiaminisha kuwa siku moja utaajiliwa Benki nikwambie unaendelea Kupoteza muda wako, tambua kuwa ajira aina mataili wala haiwezi kukufuata ulipo,"

Aidha amesema Serikali ya awamu ya tano inatambua elimu ya ufundi na ndio maana imetenga fedha kwa ajili ya kujenga vyuo vingi vya Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) ili wanafunzi wapate elimu na kuweza kujiajiri.

Naye Kaimu Mkuu wa Chuo cha VETA Dar es Salaam, Violet Fumbo amesema programu ya Vijana 2jiajiri inayosimamiwa na Benki ya KCB ni mkombozi kwa vijana wengi kwani itawasaidia kuweza kupata elimu ya ufundi stadi itakayowawezesha waweze kufanyakazi.mbalimbali za ujasiriamali.

Amesema kijana yeyote atakayepata fursa ya kupata elimu ya ufundi na ujasiriamali anapaswa kuondokana na dhana ya kuajiliwa na kuongeza kuwa VETA ipo tayari

kushirikiana na KCB ili kuweza kuwasaidia vijana kutimiza malengo yao.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya KCB,Cosmas Kimario amesema jumla ya Sh. Milioni 80 wamezitoa ili kuwasaidia vijana 123 kuwezakupata elimu ya ufundi stadi katika chuo cha VETA na baadae waweze kujiajiri.