Nyota huyo alimuita shabiki wake kwa jina Jack kujumuika naye jukwaani na kumrukia mikononi mwake- Lakini Jack hakuwa imara na wawili hao walianguka chini.

''Tulifikiri ameaga dunia,'' aliandika shabiki mmoja mtandaoni.

Badala yake, Gaga alirejea na kutumbuiza kibao chake kiitwacho Million Reasons akiwa sambamba na Jack. ''inashangaza'', ''tunapendana sana tukaanguka jukwaani pamoja.''

''Tulirukiana mikononi . Tulikuwa kama Jack na Rose wa Titanic''.

''Nafikiri tunapaswa kupata kikombe cha chai pamoja.''

Mwisho wa ujumbe wa Youtube wa Hani
Mashabiki walikuwa wakifuatilia hali ya Gaga kwa kuwa ana matatizo ya baridi yabisi hali inayomsababishia maumivu makali.

Mwaka 2013, aliahirisha onyesho lake la Born This Way baada ya kuteguka nyonga.

Lakini muimbaji huyo aliwapa moyo mashabiki wakati walinzi walipomsaidia kunyanyuka.

Gauni la Gaga lafichuliwa katika tamasha la Met Gala

Childish Gambino aweka historia katika tuzo ya Grammys

''Kila kitu kiko sawa,'' alisema. ''kitu pekee ambacho hakiko sawa ni kuwa tunahitaji ngazi ili niweze kupanda.

Pia Nyota huyo alimpa moyo Jack, ambaye alikuwa akilia baada ya tukio hilo.

''Usiwe na wasiwasi, kila kitu kiko sawa. si makosa yako,'' aliongeza: ''Unaweza kuniahidi kitu? unaweza kuacha kujilaumu kwa kile kilichotokea?''

''Alimpandisha jukwaani na kuwasihi kila mmoja mtandaoni kutomkosoa.

Baadae kwenye onyesho hilo, Gaga alithibitisha kuwa ajali hiyo haijasababisha madhara yoyote, alipotumbuiza kibao chake, Bad Romance.