Njia mpya ya utapeli yaibuka wakishirikisha Jeshi la Polisi bila kujitambua kuwa wanafanikisha dili za hawa matapeli. mfano : Matapeli wanaweza kukuuzia sim ya wizi ya bei kubwa ya kiasi cha shilingi laki nane ( 800,000/=) kwa fedha ndogo ya elfu sabini( 70,000/=) ili kukuingiza kingi ukiingia tu imekula kwako

Kwani simu hiyo unayouziwa ni ya mmoja wao (matapeli) na wanakuwa wamekopi Imei number ya simu hiyo sehemu.

Baada ya wiki wanakupigia ili kuangalia kama uko hewani. Huku wameshatoa ripoti polisi kuwa begi limeibiwa kwenye gari pamoja na vitu vingine na hiyo simu ikiwa ni mojawapo kati ya vitu vilivyoibiwa.

Na watatoa maelezo polisi thamani ya vitu vilivyoibiwa niTshs zaidi ya Milioni 7 (katika maelezo yake atakuwa ametaja laptop, fedha taslim na simu tatu au nne.)

Wanapewa mpelelezi na hapo ndipo Jeshi letu linajikuta limeingizwa kingi bila ya kujijua.

Mpelelezi anaomba msaada cyber crime kuitafuta simu hiyo.

Ikipatikana biashara inaanza . Unawekwa chini ya ulinzi kulipa vitu vyote ambavyo hujawahi hata kuviona na kesi ya wizi unayo.

Uongozi wa group unalishauri jeshi la polisi kuwa makini sana na hizi kesi za cyber. Labda mtakuja gundua kuwa simu hizi zinazotumika kutapelia watu zimekwisha ripotiwa mara mbili au tatu ndani ya miezi mitatu.

Ndugu zangu wanachama wa group hili msikubali kuuziwa simu mkononi ambayo ni used, na kama utanunua simu hiyo ambayo ni used basi mlipe kwa cheque, kagueni Imei number na umpige picha huyo aliyekuuzia pindi unapomkabidhi kiasi hicho cha Malipo.

Ikiwa hataki achana nae ndiyo salama yako.

Matapeli ni wengi sasa na wanabuni mbinu siku hadi siku ili kuyasukuma maisha yao.

Tunaitajika kuwa makini

Ahsanteni sana.