Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Kampuni ya Phoenix Tanzania (Assurance Co. Ltd) Mubaraka Kibarabara (kushoto) amkimkabidhi sehemu ya msaada wa Chakula, Nguo, Vifaa vya Shule na Fedha Taslimu, Mkuu wa Kituo cha Kulelea Watoto Yatimba cha Hisani, Hidaya Mtalemwa, wakati wafanyakazi wa Kampuni hiyo walipofika kutembelea kituo hicho kilichopo Mbagala Maji Matitu, Dar es Salaam, juzi kutoa msaada. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Fedha wa Kampuni hiyo, Godfrey Badeleya. (Picha Zote na Mafoto Media)

Mkurugenzi wa Rasilimali watu wa Kampuni ya Phoenix Tanzania (Assurance Co. Ltd) Mubaraka Kibarabara (kushoto) amkimkabidhi sehemu ya msaada wa Chakula, Nguo, Vifaa vya Shule na Fedha Taslimu, Mkuu wa Kituo cha Kulelea Watoto Yatimba cha Hisani, Hidaya Mtalemwa, wakati wafanyakazi wa Kampuni hiyo walipofika kutembelea kituo hicho kilichopo Mbagala Maji Matitu, Dar es Salaam, juzi kutoa msaada. Kulia ni Mkuu wa Idara ya Fedha wa Kampuni hiyo, Godfrey Badeleya. (kushoto) ni Meneja wa Phoenix, Robert Kalegeya.



Meneja akizungumza na watoto

Mkuu wa Idara ya Fedha wa Kampuni hiyo, Godfrey Badeleya, akizungumza

Mfanyakazi wa Phoenix Tanzania Assurance Co. Ltd, akipiga picha na mtoto wa Kituo cha watoto Yatima Hisani, wakati walipowatembelea na kutoa msaada wa Chakula, Vifaa vya Shule, Nguo na Pesa Taslimu, ambapo pia walikula nao chakula cha mchana na kufurahi pamoja.

Na Mafoto Media

KAMPUI ya Bima ya Phoenix of Tanzania Assurance Co. Ltd, imejiwekea mkakati wa kusadia watoto Yatima kila mwaka ili kuweza kusaidia na kuendeleza vipaji vya watoto waweze kufikia malengo yao.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Rasilimali watu wa Kampuni hiyo, Mubaraka

Kabarabara, wakati akikabidhi msaada wa vifaa mbalimbali vya Elimu, Chakula, Nguo na Pesa taslimu, walipotembelea katika Kituo cha kulelea watoto Yatima cha Hisani kilichopo Mbagala Maji Matitu jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, Kabarabara alisema kuwa msaada huo uliokabidhiwa katika Kituo hicho, ulichangwa na wafanyakazi wa Kampuni hiyo baada ya mmoja wao kuwasilisha wazo na kujadiliwa kwa pamoja na kisha kufanyiwa kazi mpaka kukamilika kwa zoezi hilo.

''Lilikuwa ni wazo la mmoja wetu aliyewasilisha kwetu na baada ya kujadiliana ni jinsi gani tufanye ili kulifanyia kazi, tulikubaliana na kuweza kupata michango ya wafanyakazi na kujadili vitu muhimu vya kuwasaidia watoto hawa na kuwa na makubariano ya pamoja na ndiyo maana hii leo tumeweza kulifanikisha zoezi hili,

Lakini pia baada ya kujionea na kutambua mahitaji ya watoto hawa bado ni mengi na muhimu tumejiwekea utaratibu wa angalau kila mwaka tuwe tukifanya zoezi kama hili hata mara moja ila tukifanikisha zaidi angalau tuweze kufanya hivi kula na kufurahi na watoto mara mbili kwa mwaka. alisema Kabarabara

Mwishoni mwa wiki Wafanyakazi wa Kampuni ya Phoenix walifika katika Kituo hicho na kukabidhi msaada, ambapo pia walipata fursa ya kula chakula cha mchana pamoja na watoto wa kituo hicho cha Hisani chenye jumla ya watoto 40 wa kike wakiwa ni 19 na wa kiume 21.

Akitoa shukrani zake kwa Kampuni ya Phoenix, Mkuu wa Kituo hicho, Hidaya Mutalemwa, aliwashukuru wadau wa Kampuni ya Phoenix waliojitolea kufika na kutoa msaada kwa watoto wa kituo hicho chenye changamoto nyingi ambazo kuisha kwake kunategemea wadau mbalimbali.

''Hatuna neno zuri la kusema ili mtuelewe tunawashukuru kwa kiasi gani, ila mungu awabari kwa hiki mlichokitoa kwa watoto wetu leo wamefurahi kiasi wengine wanawalilia msiondoke muendelee tu kubaki nao, Changamoto ni nyingi katika kituo hiki ambazo nyingi zinategemea wadau kama ninyi ili watoto waendelee kuishi kwa amani na furaha kama hii leo''. alisema Hidaya.

Picha ya pamoja....