Ester Kiama aliyekuwa akishangaa wanaume kutomtamkia ndoa licha ya kukiri Kama ni uzuri amejaaliwa, kwasasa imebainika tayari ameshapachikwa mimba lakini anajifichaficha ambapo alipoulizwa kuhusu hilo amejibu .
“Yaani kwa sasa sihitaji picha za kuonesha tumbo langu kama wanavyofanya wengine wala kuonekana mitaani kwa sababu mimba yangu siyo fasheni, hiki ni kiumbe, kipo ndani ya tumbo, kinahitaji heshima maana wengine wana macho ya husda hivyo ni vizuri tukaishi kama wazee wa zamani maana hawakuwa na Snapchat wala Instagram,” Actress huyo amefunguka