Ni kawaida katika miji mikubwa yenye msongamano wa watu katika nchi nyingi barani Afrika kukumbwa na adha ya usafiri wa raia wake.

Nchini Tanzania, hali hiyo inaweza kuonekana zaidi katika majiji makubwa kama Dar es Salaam, Mwanza na Arusha, ambapo shida ya usafiri upelekea watu kujazana kwenye usafiri wa daladala ambao ndio unawapa unafuu watu wengi.

Kero kubwa ambayo imetajwa kuwachosha wanawake wengi kwenye daladala ni tabia ya baadhi ya wanaume kukaa nyuma yao, maarufu kwa jina la 'Kubambia', hali inayowafanya kukosa amani katika usafiri.

Kupitia mada iliyowekwa katika ukurasa wa Facebook wa EATV, wanawake wengi waliotoa maoni yao wameonesha kukerwa na tabia hiyo, huku wengine wakidai kuwa baadhi ya wanaume hufanya makusudi ili tu waweze kutimiza haja zao.