Rais wa Tanzania, John Magufuli kesho Ijumaa Juni 7, 2019 atakutana na wafanyabiashara watano kutoka kila Wilaya kujadili mambo mbalimbali.

Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi Juni 6, 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa imesema mkutano huo utafanyikia Ikulu kuanzia saa 3.30 asubuhi.

Msigwa amesema wafanyabiashara hao watawawakilisha wenzao ambapo wataambatana na wajumbe wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC).

“Mkutano huu utaanza saa 3:30 asubuhi hivyo wajumbe wote wanatakiwa kuwasili katika ukumbi wa Kikwete kuanzia saa 2:00 hadi saa 2:30 asubuhi,”  amesema Msigwa.