MWANAMITINDO maarufu duniani Kim Kardashian ameamua kumuonyesha mtoto wake wa kiume kwa kuweka picha kwenye mtandao wake wa instagram kwa mara ya kwanza.

Mwanamitindo huyo kwenye kipindi chake cha runinga ‘Keeping up with Kardashians’, Kim Kardashian, alimuonesha mtoto wake huyo aliyezaliwa mwezi mei kwa njia ya mama mbadala na kumpatia jina la Psalm West.


Kim Kardashian ameweka picha ya mtoto huyo ikiambatana na ujumbe uliosomeka, ‘Psalm Ye’ Psalm likiwa na maana ya Zaburi.