Maafisa nchini Sudan kwa mara ya kwanza wamethibitisha kuwa hali siku ya juma wamekanusha madai kuwa watu 100 waliuawa na wanajeshi wakati wa maandamano na kukiri kuwa ni watu 46 waliyouawa katika purukushani hilo.

Madaktari wanaohusishwa na vuguvugu la waandamanaji wanasema idadi ya watu waliouawa na vikosi vya usalama wiki hii imepanda na kufikia zaidi ya watu 100.

Walisema miili 40 iliopolewa kutoka mto Nile mjini Khartoum siku ya Jumanne.


Awali mamlaka ilikuwa kimya kuhusiana na suala hilo lakini,maafisa wa wa wizara ya usalama mapema siku ya Alhamisi ilisema idadi ya waliyofariki ni 46.

Wanaharakati wa upinzani nchini Sudan wamekataa wito wa kufanya mazungumzo na baraza la kijeshi, ukihoji kuwa baraza haliwezi kuaminika baada ya msako wa nguvu dhidi ya waandamanaji.

Wakaazi wameiambia BBC kuwa wanaishi kwa uwoga katika jiji kuu la Khartoum.

Naibu mkuu wa Bwaraza hilo la Jeshi amepinga madai ya ukandamizaji na kuongeza kuwa wahalifu na walanguzi wa dawa za kulevya walikuwa wamejipenyeza katikati ya waandamanaji hao kufanya biahara zao.

"Hatutakubali vurugu kutokea na kamwe hatutarejea nyumakatika msimamo wetu. Hatuwezi kurudi nyuma. Lazima tuhakikishe nchi inaongozwa kwa utawala wa sheria," alisema Mohammed Hamadan - ambaye pia anafahamika kama Hemedti - siku ya Jumatano.

Ripoti kadhaa kutoka mjini Khartoum zinaarifu kuwa kikosi maalum cha kijeshi kinachojulikana kama Rapid Support Forces (RSF), kimekuwa kikifanya msako katika barabra kadhaa za mji huo na kinawalenga raia.

Kikosi hicho zamani kilijulikana kama wanamgambo wa Janjaweed, na kinasadikiwa kuhusika na mauji na ukatili katika mzozo wa Darfur Magharibi mwa Sudan mwaka 2003.


Viongozi walioongoza vuguvugu la kutaka utawala wa kiraia kuongoza nchi hiyo, wamesema wamesitisha mawasiliano na serikali ya mpito ya kijeshi na kufanya mgomo.

Vikosi vya usalama vilifika maeneo ambayo watu walikua wakiandamana, mapema Jumatatu na sauti za risasi zilisikika kwenye picha za video.

Chanzo ni nini?
Waandamanaji wamekua wakikita kambi nje ya jengo la makao makuu ya jeshi tangu tarehe 6 mwezi Aprili, siku tano kabla ya kuangushwa kwa utawala wa Bashir.

Mwezi uliopita, waandaaji na majenerali watawala walikubaliana kuhusu muundo wa serikali mpya na muda wa mpito wa miaka mitatu kuelekea kwenye utawala wa kiraia.

Hawajaweza kuamua kuhusu ni upande upi hasa kati ya raia au jeshi kuchukua nafasi nyingi zaidi.