Mbunge wa Kawe kupitia CHADEMA, Halima James Mdee, amewashukuru Watanzania kwa maombi yao pindi alipokuwa akiugua, huku akiwajulisha hali yake inavyoendelea kwa sasa.


Halima Mdee ameandika ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa twitter na kusema kwamba hivi sasa amesharuhusiwa kutoka hospitali hivyo yupo nyumbani kwake, na anendelea vizuri kiafya.

 "HABARI za asbh Wakuu. Kwa heshima kubwa, naomba niwashukuru WOTE kwa MAOMBI na SALAMU za POLE. Nimeshatoka HOSPITAL na AFYA yangu INAIMARIKA kwa KASI ya AJABU. Sina cha kuwalipa kwa UPENDO wenu MKUU, Mungu AWASIMAMIE na KUWABARIKI katika KILA JAMBO MNALOLIFANYA. 🙏🏿 sana."


Jumamosi ya Juni 9, zilitolewa taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Bw. Joh Mrema, kuwa hali ya Halima Mdee haipo sawa kutokana na kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kutolewa uvimbe tumboni.