Shirika moja la udhibiti wa matibabu nchini Canada limempokonya rasmi leseni daktari mmoja wa rutba ya uzazi aliyestaafu ambaye alitumia mbegu zake za kiume kuwapatia ujauzito wanawake wasioweza kushika mimba.Dr Norman BarwinMalalmishi yaliowasilishwa yanadai kwamba Dkt. Norman Barwin aloitumia mbegu zake za kiume kuwashikisha ujauzito wagonjwa wake

Chuo kikuu cha madaktari wa maungo na upasuaji cha Ontario kilitaja vitendo vya daktari Norman Barwin kuwa vya ‘aibu kubwa’.

Shirika hilo lilianzisha uchunguzi kuhusu madai dhidi yake mwaka 2016. Madai hayo yalianzia mwaka 1970 na yanashirikisha wagonjwa kutoka kliniki mbili za rutba ya uzazi mjini Ontario.

Akizungumza kwa niaba ya bodi ya jopo la nidhamu katika shirika hilo mjini Toronto siku ya Jumanne, bwana Steven Boldley alisema kuwa ya shirika hilo kwa bahati mbaya halikuweza kumchukulia hatua kali daktari huyo isipokuwa kumpokonya leseni yake mbali na kumtoza faini.

”Ulisaliti uaminifu wa wagonjwa wako na kupitia vitendo vyako uliathiri watu binafsi na familia zao na kusababisha uharibifu mkubwa ambao utaendelea kuwepo kwa vizazi vijavyo”, alisema.

Akiwa na umri wa miaka 80, daktari Barwin hakuwepo mbele ya jopo hilo la nidhamu na aliwakilishwa na wakili wake.