Naibu waziri wa ulinzi nchini Marekani Patrick Shanahan alisema kuwa Marekani ilifanya busara sana


Kaimu waziri wa ulinzi nchini Marekani Patrick Shanahan alisema kuwa Marekani ilifanya busara sana
Mashambulio yaliopangwa na Iran yamezuiwa na vitendo vya Marekani kulingana na naibu waziri wa maswala ya ulinzi nchini Marekani Patrick Shanahan.

Marekani imeonya kuhusu tishio kutoka kwa Iran katika wiki za hivi karibuni na bwana Shanahan aliwaelezea wabunge katika mkutano wa faragha.

Hali ya wasiwasi imeongezeka huku Marekani ikipeleka vifaa vya kijeshi katika eneo la mashariki ya kati ili kukabiliana na vitisho hiyo visivyojulikana.


Amesisitiza sera mbaya dhidi ya Iran na tangu alipochukua mamlaka mwaka uliopita aliiondoa Marekani kutoka katika mkataba wa Kinyuklia na Iran pamoja na mataifa mengine matano yenye uwezo mkubwa duniani.

Mshauri wa maswala ya usalama nchini Marekani John Bolton amekuwa akipigania kubadilishwa kwa utawala wa Iran na amekuwa akitoa wito kwa Marekani kuilipua nchi hiyo.


Akizungumza na waandishi wa habari , alisema kuwa lengo la Marekani ni kuzuia badala ya vita.

Bwana Shanahan ambaye aliwahutubia wabunge akiwemo waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Mike Pompeo alisema: Nadhani hatua zetu zilikuwa za busara na tumezuia mashambulio dhidi ya Marekani na hilo ndio muhimu.

''Naweza kusema kuwa tuko katika muda ambao vitisho viko juu na kazi yetu ni kuhakikisha kuwa hakuna uharibifu wowote utakaofanywa na Iran''.

Hakutoa maelezo yote kuhusu habari hizo muhimu zinazohusiana na swala hilo , lakini akaongezea: Natumai kwamba Iran inasikiliza.

Tupo katika eneo hili ili kuzungumzia mambo mengi, lakini sio kupigana na Iran.

Ripoti zinasema kuwa hotuba hiyo ilikumbwa na pingamizi mara nyengine na baada ya mkutano , baadhi ya wabunge wa chama cha Democrats waliwashutumu maafisa wa serikali kwa kubadilisha habari za kijasusi.

Kwa maoni yangu , hakukuwa na habari yoyote kwa nini tunapaswa kuanza mazungumzo ya kivita na Iran, alisema mbunge wa chama tawala Ruben Gallego.

Iran ilikubali kwamba kundi la JCPOA litapunguza mipango yake ya kinyuklia huku Iran nayo ikifaidika kwa kuondolewa vikwazo 2015 , na imeyataka mataifa ya magharibi kuheshimu mkataba huo licha ya Marekani kujiondoa.



Maafisa wa Iran walisema siku ya Jumatatu kwamba wameongeza kiwango cha uzalishaji wa madini ya Uranium -ijapokuwa ongezeko hilo ni la muda na ndani ya masharti ya makubaliano hayo.