BAADA ya kutwaa ubingwa jana, mabingwa wa Ligi Kuu Bara Simba leo wanarejea makao makuu ya klabu Msimbazi kuendeleza sherehe za ubingwa.

Sherehe za ubingwa zitaanzia maeneo ya Kibaha, mkoani Pwani majira ya saa 5:30 ambapo wachezaji pamoja na kombe watapanda gari la wazi kuwaonyesha kombe mashabiki wao.

Mchezo wao wa mwisho jana walikubali suluhu mbele ya Mtibwa Sugar mchezo uliochezwa uwanja wa Jamhuri, Morogoro.